• Thu. May 2nd, 2024

Asasi za Ulinzi zalalamikia Kuaibishwa kwa polisi na Gazeti Moja Nchini

Oct 22, 2021
Riot police patrol during a protest in Kibera Slums, Nairobi, Kenya, Monday May 23, 2016. The protests, held every Monday for the past four weeks, come before elections next year and are organized by Kenya's main opposition group the Coalitions for Reforms and Democracy. (AP Photo/Sayyid Azim)
561 300

Kitengo cha Upelelezi wa Jinai, DCI kimetoa habari za kufedheheshwa na ujumbe uliochapishwa na gazeti moja humu nchini unaopania kuiharibia Jina Idara ya Polisi.

“Gazeti hilo ambalo kichwa chake cha habari ilikuwa”NJAA YAUMA POLISI BAADA KAFYU KUISHA” ni fedheha kwa shirika linalotegemewa na wananchi kwa kutoa habari tendeti na za kujenga kuchapisha taarifa zisizokuwa na msingi wala maadili hususan kuiharibia Jina idara ya Polisi,” walisema katika Taarifa.


Idara hiyo imesema kuwa mbali na kuwepo kwa maafisa wachache wa usalama wanaoenda kinyume na maadili ya kazi ya Polisi, hiyo haijatosha kuwa sababu kuipaka matope idara nzima ya usalama.

Idara ya DCI imesema kuwa asilimia kubwa ya maafisa wa usalama wanafanya kazi yao kwa ustadi unaohitajika.


“Itakuwa vyema iwapo mashirika ya kutoa habari yatakuwa makini kutoa taarifa za ukweli na zenye manufaa kwa wananchi na wala sio habari za uchochezi na kupotosha zinazojenga taswira mbaya kati ya maafisa wa usalama na wananchi kwa jumla,” walisema


Aidha wamesema kuwa Idara ya Polisi iko imara na itaendelea kumlinda mwananchi na kutekeleza majukumu yake ipaswavyo kwa mujibu wa sheria.

READ ALSO:Mbunge Akamatwa na Kufikishwa Makao Makuu ya DCI

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *