• Fri. Apr 26th, 2024

Afisa wa polisi akamtwa baada ya kumpiga mkewe

Jun 10, 2021
Tired frustrated african wife ignoring angry black despot husband arguing blaming upset woman of problems, jealous man shouting at sad girlfriend, family fight and controlling boyfriend, disrespect
229 300

Afisa wa Polisi anayefanya kazi katika kituo cha Kacheliba eneo bunge la Pokot Kusini ameshtakiwa katika kituo cha Polisi Lwakhakha baada ya kumpiga mke wake na kifaa kisicho julikana kwenye kichwa.

Afisa huyo kwa jina Isaac Ochome Otwane ambaye hakuwa kazini siku hiyo alikuwa na ubishi na mkewe Linet Sikuku Ndiema mwenye umri wa miaka 43 na ndipo alipompiga kichwani kwa kifaa kisicho julikana na akapoteza fahamu.

Mwanamke huyo alikimbizwa katika hospitali ya kaunti ndogo ya Cheptais anapoendelea kupata matibabu.

Hali yake japo si nzuri. Aidha mshukiwa alikamatwa na maafisa wa kituo cha lwakhakha na atashtakiwa kwa kosa la kumdhulumu na kumuumiza mke wake.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *