Spika Wa bunge la kaunti ya Nairobi Ben Mutura ametupilia mbali jaribio la mageuzi ya uongozi wa wachache ambapo Peter Imwatok anadaiwa kuondolewa kama Kiranja wa wachache .
Kulingana na barua kutoka kwa Mutura bwana Imwatok ndiye kiranja halisi upande wa wachache na kwamba jaribio la kumtoa lilifanywa kinyume na sheria za bunge.
‘‘Hii ni kudhibitisha kuwa nilipata barua kutoka kwa chama cha ODM kikisema kuwa kuwa hakijafanya mabadiliko yoyote katika uongozi wake katika bunge hilo na kwamba pia nakubuliana na naibu kiranja wa wachache Moses Ogeto kuwa sheria haikufuatwa kumwondoa Imwatok,’’ Mutura alisema.
Hayo yakijiri chama cha ODM kupitia katibu wake Edwin Sifuna kimeweka wazi kuwa watafanya mkutano leo na kuwapa barua wakilishi wadi kaunti ya Nairobi waliohusika katika jaribio hilo kwani hata baada ya kukomeshwa na chama hawakutii.
Sifuna alisema, ‘‘tumechoka na sarakasi za wakilishi wa chama na ni nkweli tutafanya mkutana na kuwapa barua za kinidhamu.’’