• Fri. Apr 26th, 2024

Senegal Waeleza Dhamira yao ya Kushinda Kombe la Bara Afrika

Feb 5, 2022
453 300

Sadio Mane na Edouard Mendy wanasema Senegal imedhamiria kupunguza shinikizo kwa kocha Aliou Cisse kwa kushinda Kombe la Mataifa ya Afrika siku ya Jumapili.

Senegal, washindi wa pili wa Kombe la Mataifa ya Afrika mwaka wa 2019, walikuwa miongoni mwa timu zilizopigiwa upato kabla ya michuano hiyo, lakini walistahimili mwanzo wa polepole nchini Cameroon.

“Ninaamini mtu huyu [Aliou Cisse] anastahili kila kitu kwa sababu ndiye kocha aliyekosolewa zaidi kuwahi kuona maishani mwangu, lakini hakati tamaa,” Mane aliambia BBC Sport Africa.

“Anajiamini, analiamini kundi. Ana wakosoaji nje, lakini hapa anafanya kazi yake. Muhimu zaidi, tungependa kushinda hii kwa ajili yake na nchi yetu kwa sababu anastahili baada ya yote aliyopitia kama mchezaji wa Senegal na sasa kama kocha.

“Itakuwa thawabu kubwa kwa kila kitu ambacho ametoa kwa nchi yake.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *