Mwanabiashara shupavu katika jiji la Nairobi Agnes Kagure sasa ametangaza wazi kuwa atawania kiti cha ugavana Nairobi mwaka ujao.
Kagure ametangaza hii leo katika mkutano wa Azimio la Umoja kule kaunti ya Nyeri mbele ya umati na wazee wa jamii ya Agikuyu.
Kagure alikua amendamana na kiongozi wa ODM Raila Odinga pamoja na mama Idah Odinga wakati wa hafla hiyo.
Sasa anaungana na Tim Wanyonyi pamoja na Margret Wanjiru katika kinyanganyiro hicho cha ugavana Nairobi.
Bado hajaweka wazi kuwa atawania kiti hicho kupitia chama gani japo kuna fununu kuwa huenda akaingia ndani ya chama cha ODM.
‘‘Kwa wakenya wote sisi tuko salama kwa mkono wa baba kama rais wetu lakini Mlima Kenya iko salama mkononi mwa Agnes Kagure kama gavana na hivi karibu nitazindua rasmi azma yangu ya ugavana.’’ Kagure alisema.