Mwili wa mwanamume mwenye umri wa makamo umepatikana baharini, baada ya jamaa huyo kudaiwa kujirusha kutoka kwenye daraja la Kilifi jioni ya jana
Kulingana na maafisa wa polisi waliopata taarifa kutoka kwa kitengo cha usalama wa baharini, jamaa huyo alipatikana akiwa amefariki, baada ya kujitupa kutoka juu ya daraja hilo, na kisha kugonga mawe kabla ya viungo vyake kadhaa kuvunjika na kufariki papo hapo
Akithibitisha kisa hicho Esther Mwendwa, ambaye ni naibu kamanda wa polisi eneo bunge la Kilifi Kaskazini ameeleza kuwa, mwili wa jamaa huyo ambaye haujatambulika kufikia sasa, unaendelea kuhifadhiwa katika hifadhi ya maiti ya hospitali ya Rufaa ya Kilifi
PHOTOS: Padme initiative-Kilifi Chapter
Kamanda huyo aidha amewataka wananchi kuchukua hatua za kutafuta ushauri nasaha, endapo yeyote ametatizikia kiakili, haswa wakati huu mgumu wa maisha, ili kuzuia visa kama hivi kutendeka
Polisi wameanzisha uchunguzi kutambua kiini cha kisa hicho