• Tue. Apr 22nd, 2025

Taarifa News

Latest News Around the Globe

Polisi Wamzuilia Mhubiri Tapeli Likoni,Mombasa

Jan 21, 2022
619 300

Polisi katika eneo la Likoni wamemtia mbaroni mwanamume mmoja anayedai kuwa nabii na anafanya miujiza ya kuponya watu magonjwa na matatizo mengine.

Laban Mwangi wa kanisa la Jesus Winners Ministry Likoni anadaiwa kuwalaghai waumini wake maelfu ya pesa akidai kuwaponya matatizo yao yakiwemo utasa, kukosa kazi na magonjwa mengine.

Akithibitisha kukamatwa kwake mkuu wa polisi wa Likoni Joseph Karanja amesema kuwa haya yanajiri baada ya wanawake 7 kupiga ripoti kudai kulaghaiwa kwa ahadi kuwa wangeponywa kupitia miujiza.

Wanawake hao wakisema kuwa wanauza hadi vyombo vyao vya nyumbani kutafuta miujiza hiyo.Kwa sasa anazuiliwa na polisi akisubiri kufikishwa mahakamani.

READ ALSO:Dutch National Nabbed By DCI Over Human Trafficking

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *