• Mon. Apr 28th, 2025

Taarifa News

Latest News Around the Globe

Muhamaji Haramu Afaulu Kuwa Hai baada ya Masaa Saba ya Usafiri

Jan 24, 2022
633 300

Muhamiaji haramu akiwa amejificha kwenye sehemu ya gurudumu la pua la ndege ya mizigo iliyokuwa ikielekea Amsterdam alipatikana akiwa hai na mamlaka ya Uholanzi Jumapili asubuhi.

Mamlaka inashuku kuwa mwanamume huyo alijificha kwa zaidi ya saa 11, akikabiliana na hali mbaya ya hewa.

Ndege hiyo ilikuwa imetoka Johannesburg, Afrika Kusini, ilisimama Nairobi, Kenya, kabla ya kuanza kuelekea Uwanja wa Ndege wa Schiphol mjini Amsterdam.

Maafisa bado hawajatambua utambulisho wa mwanamume huyo lakini wanaamini kuwa anaweza kuwa na umri wa kati ya miaka 16-35.

Pia wanachunguza iwapo alipanda ndege hiyo kutoka Johannesburg au Nairobi.Walipofika katika eneo la tukio, polisi wa Uholanzi na wahudumu wa dharura walithibitisha kwamba mtu huyo alikuwa hai.

Walakini, alikuwa na joto la chini la mwili.Mtu huyo alisaidiwa kuamka na kisha kusafirishwa hadi hospitali ya Amsterdam anakopokea mitabu.

Mnamo Februari mwaka jana, mvulana Mkenya mwenye umri wa miaka 16 alinusurika joto la chini ya sifuri kwenye safari ya saa moja kutoka London hadi Uholanzi kwa kujificha karibu na vifaa vya kutua vya ndege.

Alianza safari yake jijini Nairobi na kutoka huko hadi Istanbul, Uturuki, kabla ya kuendelea na kutua Uwanja wa Ndege wa London Stansted.

Alitibiwa kwa hypothermia na akapata ahueni kamili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *