• Sat. Apr 20th, 2024

Wahudumu wa Afya NMS Watishia Kushiriki Mgomo Wakidai Mshahara

Aug 12, 2021
265 300

Wahudumu wa afya Nairobi chini ya usimamaiza wa NMS wametishia kushiriki maandmano ikiwa hawatapokea mishara yao ya mwezi Julai siku mbili zijazo.

Katibu mkuu wa chama cha wauguzi nchini KNUN tawi la Nairobi Boaz Onchari anasema kuwa wahudumu wa afya hawajapokea mishahara yao ya mwezi Julai na viongozi wa kitengo cha NMS wamewapa mgongo na mpaka sasa hawajui ni lini wanapokea pesa zao.

‘‘Tulifanya makubaliano nao kuwa kufikia tarehe tano wawe wanalipa mishahara lakini kwa sasa hatujui ni vipi hili limekiukwa na tumesalia tukihangaika huku  mabosi hao wa NMS wakiendelea kutupuuza…tuna watoto tunahitaji kulipa kodi za nyumba wanataka tufanye vipi,’’ Boaz aliambia wanahabari

viongozi wa Wahudumu wa Afya katika Kikao na Wanhabari PICHA/Jacktone

Pia wameshtumu utendakazi wa NMS wakitaka rais Uhuru Kenyatta kuingilia kati la sivyo wako tayari kurejea katika uongozi wa serikali ya kaunti.

‘‘NMS iliapa kulinda haki zetu kwa sasa ni mwezi kumi na sita na hakuna cha mno cha kuzungumzia tukiangalia maisha ya wafanyikazi ni shida tupu na tuko tayari kurudi kwa serikali ya kaunti..hata mama anaweza.’’ Onchari aliongeza.

Brown Ashira wa chama cha wahudumu wa afya khps kwa upande wake amesema kuwa ikiwa siku hizo mbili zitakamilika bila kupata mishahara basi wataingia barabarani kushinikiza NMS kulipa fedha hizo

‘‘Hatutakaa chini na kuwatazama tukiwa njaa,baada ya siku mbili tutajitokeza wahudumu wote  na tuingie kwenye maandamano.’’ Alisema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *