• Fri. Apr 19th, 2024

Viongozi Wataka Raila na Kalonzo Kuungana Uchaguzi wa 2022

Aug 30, 2021
422 300

Baadhi ya viongozi wa kisiasa  kule Embakasi South Nairobi sasa wanataka kinara wa ODM Raila Amollo Odinga kuendelea kushirikiana na kiongozi wa Wiper Kalonzo Musyoka katika siasa za kitaifa mwaka wa elfu 2022.

Mwakilishi wadi wa Kware Rose Kula  anasema  viongozi hao wawili wana mtazamo mzuri kwa taifa na ipo haja  ya wao kufanya kazi pamoja tena.

‘‘Naomba kama mwanamke na kwa unyenyekevu wa nchi hii, kaa na baba yangu Raila Amollo Odinga mtupe mwelekeo…Mimi kama Rose nikiona uko kando na Raila yuko Kando basi Nina mshutuko ..kwa sababu hii wakenya wa kawaida wako wengi kuliko wale wanalia.” Rose alisema.

Raila na Kalonzo Katika Mkutano wa Kisiasa

 ‘‘Ukienda ukae chini nione umetupatia mwelekeo hata hapa chini mashinani Mwananchi wa kawaida atakua na mwelekeo.”aliongeza

Walikuwa wanazungumza katika kanisa moja kule Embakasi South hafla ambayo ilihudhuriwa na viongozi mbali mbali sehemu hiyo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *