• Fri. Apr 19th, 2024

Utumizi wa basi za shule kwa matanga wapigwa marufuku

Jun 15, 2021
724 300

Kamishna wa eneo la Nyanza Magu Mutindika amepiga marufuku utumizi wa Magari ya shule na kanisa katika shughuli za Mazishi na harusi katika eneo hilo.

Kulingana na kamishna huyo hii ni mojawapo ya njia za kupunguza kuenea kwa maambukizi ya virusi vya Korona.


“Kutokana na kupanda kwa idadi ya wanapoambukizwa virusi vya Korona, mabasi ya shule, vyuo na kanisa zisitumike katika kuwasafirisha watu kwenye harusi au matanga,” alisema Magu


Maafisa wa Polisi wameelekezwa kuhakikisha hakuna gari lolote la shule linatumika kama ilivyoagizwa.


“Mtahakikisha masharti haya yanafuatwa mpaka maagizo mengine yatakapotolewa,”aliongeza Magu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *