Baraza la walemavu nchini Sasa limeaanda kikao na washika dau mbali mbali wa maswala ya sheria ili waweze kuskuma huduma zao Mtaani ikiwemo maswala ya sheria, yanayakumba walemavu na hata uhamasisho wa haki zao.
Baraza hilo, Shirika la Sheria Mtaani, Ofisi ya Ombudsman,Shirika la Fida yote yamekongomana Tononoka Grounds Mombasa ambako wanaangazia haki na Huduma mbali mbali Kwa jamii hiyo inayoishi na ulemavu.
Wakili Shadrack Wambui ambaye ni mwanzilishi wa shirika la Sheria Mtaani.
‘‘Tuko hapa Mombasa pamoja na mashirika mengine kama vile FIDA ,Ofisi ya Ombudsman tuko hapa ajenda kubwa ni kuweza kushughulikia wananchi katika maswala ya sheria,haki zao haswa walemavu..tuko mpaka kesho siku ya Alhamisi.’’ Wambui alisema.
Wananchi poa watapata nafasi ya kupokea huduma hizo.