• Thu. Apr 25th, 2024

Polisi  Waonya Kuhusu Wanaokiuka Kanuni za Kafyu Nairobi

Aug 2, 2021
239 300

Polisi hapa Nairobi wametaka wananchi kufuata kanuni za Covid 19 haswa kafyuu kwani hawatalegeza kamba katika juhudi zao za kuhakikisha  kanuni  hizo zinafwatwa.

Wengi walijipata pabaya Jumamosi hii ni baada ya barabara kuu ya Thika  kuwekewe vizuizi baada ya saa nne usiku.

Kulingana na kamanda wa polisi Kasarani Peter Mwanzo wataendelea  kuweka roadbloaks hizo, kuhakikisha kuwa wale wanaokiuka sheria wanaandamwa.

‘‘Tulipata mwelekeo kuwa aina ya ugonjwa huu sasa ni hatari na ni lazima wakenya wafwate masharti na kanuni zote za ugonjwa huu na kwamba sisi tuendelea kuhakikisha kuwa tumewandama watakaokikua sheria hizo.’’ Mwanzo alisema.

Maafisa wa Polisi Wakiweka Vizuizi Jumamosi Thika rd 31/7/2021 PICHA/MKATABA

Ameongeza kuwa imekuwa vigumu kudhibiti barabara hiyo ya Thika road kwa sababu ya uzembe na kutosikia kwa wakenya huku wengi wakikosa kuheshimu kanuni za Covid, haswa masaa ya kafyu.

‘‘Wakenya ni wasumbufu sana ukizingatia msongamanoi ulishuhudiwa ni watu ambao hawaskizi na hawaelewi chochote..lakini hatutakoma tutaendelea kuweka vizuizi na wanaotoa hudumu  muhimu tutawelekeza.’’ Mwanzo aliongeza.

Msongamano ulishuhudiwa katika barabara ya Thika siku ya Jumamosi  baada ya polisi kuweka vizuizi kadhaa katika barabara hiyo.

Ilimlazimu kamanda wa polisi Nairobi Augustine Nthumbi kufika katika eneo hilo kakagua hali baadae vizuizi hivyo vilitolewe.

Wiki jana inspekta mkuu wa polisi Hilary Mutyambai aliotoa amri kwa jeshi la polisi kuhakikisha kuwa kanuni zote za Covid zimefwatwa kikamilifu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *