• Wed. Apr 24th, 2024

Mbunge Akosoa Serikali Kwa Kuchelewa Kwa CDF

Jan 26, 2023
346 300

Mbunge wa Malindi bi Amina Mnyanzi ameilaumu serikali kwa kile anachodai kwamba ni hujuma kwa jitihada za masomo kwa kukosa kueka Hela za mgao wa CDF kama ilivyohaidi bilioni mbili baada ya Kila majuma mawili

Akiongea na kikao cha wanahabari mjini Mombasa katika kongamano la wabunge Bi Amina aidha amesema kwamba kukosa kuenda shule kutachangia pakubwa kwa wanafunzi kupata mimba za mapema napia kuchangia mahisiano potovu ya jinsia mmoja.

.Takriban wanafunzi alfu kumi na tano katika eneo bunge la Malindi wanategemea ufadhili wa CDF,

Hata ivo mapema hii Leo serikali imeingilia kati na kusitisha mgomo wa wabunge ambao wamesusia vikao vyote tangu kuanza kwa mkutano huo na kuahidi kima Cha shilingi milioni thelathini na nne kwa Kila eneo bunge ambayo ni nusu ya millioni mia Moja wabunge walizoitisha kabla ya kurejelea vikao vya kongamano hilo

Kupitia spika wa bunge Moses Wetangula,Rais William Ruto amewarai wabunge kusitisha mgomo wao na kurejelea vikao vya kongamano uku akisema serikali yake italipa Hela izo Kila juma uku akisema Kenya Ina madeni mengi sana kama lile la uchina ambalo serikali imelipa shilingi bilioni sitini na nane siku ya jana.

Rais Ruto anatarajiwa katika eneo la pwani siku ya juma tatu wiki ijayo kufungua rasmi kongamano hilo la wiki mbili.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *