• Wed. Apr 24th, 2024

Mawakili Wapongeza Kuzimwa Reggae ya BBI

Aug 21, 2021
300 300

Mawakili sasa wameendela kutoa hisia mbali mbali kuhusu uamuzi wa jana wa BBI huku wengi wakipongeza  mahakama ya rufaa  kwa uamuzi huo wakisema kuwa katiba imelindwa.

Akizungumza na TaarifaNews  wakili Shadrack Wambui anasema kuwa kulikuwa na njama fiche ya kuteka nyara idara ya mahakama kupitia BBI, na kwamba mwananchi hakuhusishwa kikamilifu.

‘‘Kwana uamuzi huo ni wa kihistoria majaji wameeleza bayana kuwa sheria haikufwatwa…mimi kama wakili nakubuliana nayo na ni kweli uhamasisho haukufanywa kikamilifu na mchakato mzima ulikuwa unaendeshwa na wanasiasa,’’ alisema.

‘‘Rais mwenyewe alikula kiapo kulinda katiba yeye mwenyewe hafai tena kuskuma mabadiliko yake,lazima tulinde katiba yetu na  mapendekezo hayo mengi yalikuwa kinyume na sheria.’’ Aliongeza.

Wakili Shadrack Wambui Baada ya Kikao Katika Mahakama ya Milimnai Nairobi PICHA/Maktaba

Kusonga ametaka wakenya kuwacha katiba kuhudumu na wanaisiasa wanafaa kuwa waaminifu na kuitumikia.

‘‘Kusonga mbele ni kwamba lazima tulinde katiba yetu ikiwa kuna wale wanaotaka kuibadilisha basi wafuate sheria.’’ Wambui alisema.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *