414 300
Jamaa mmoja anayetambuliwa kwa jina Allan Owino Oremo ameripti kupoteza pochi lake akiwa ameabiri gari la Kampuni ya Embassava.
Mwanaume huyu amesema kuwa alikuwa anasafiri kutoka katikati mwa jiji kuelekea Mtaa wa Fedha kule Embakasi.
Pochi hilo lilikuwa na stakabadhi zake kama vile, Kadi ya matibabu ya Kampuni ya ndege ya Kenya [KQ], Kadi ya Benki, Kitambulisho cha taifa na Kadi nyinginezo. Aidha pia shilingielfu nne mia tano zilikuwemo.
Visa vya abiria kupoteza na kuibiwa wakiwa kwenye matatu vimekuwa vikiripotiwa sana katika matatu za humu Jijini Nairobi.